• complaint |
    • Wasiliana nasi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
ASSOCIATION OF LOCAL AUTHORITIES OF TANZANIA-ALAT
ASSOCIATION OF LOCAL AUTHORITIES OF TANZANIA-ALAT

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania

  • Home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
  • Tunafanya nini?
    • Service one
    • Services two
  • Utawala
    • Organization Structure
  • Machapisho
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Utawala
    • Application Forms
  • Kituo cha Habari
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • Habari Mpya
    • Matukio
  • Projects
    • lic projects
  • Halmashauri

Rais Samia Aziagiza Halmashauri Kusimamia Mapato na Matumizi Sahihi

Posted on: March 13th, 2025


Na Mwandishi Wetu,Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameziagiza halmashauri zote nchini kusimama imara na kuwa makini katika ukusanyaji wa mapato pamoja na matumizi yake ili kuhakikisha fedha za umma zinatumika kwa njia sahihi.

Akifungua Mkutano wa 39 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) jijini Dodoma, Rais Samia amewaonya viongozi wa halmashauri dhidi ya ubadhirifu wa fedha za serikali, akimuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Mhe.Mohamed Mchengerwa, kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha na kuchukua hatua kali dhidi ya watumishi wanaoiba au kughushi risiti za mapato.

“Kama mmewabaini hawa watu walioghushi risiti, tafadhali sana, lile jicho lenu la huruma hapa hapana,” ameonya Rais Samia, akisisitiza kuwa viongozi watakaoshindwa kuwachukulia hatua wahusika watawajibishwa wao wenyewe.

Pia amekemea vikali urasimu unaokwamisha wawekezaji, akiwataka viongozi wa halmashauri kuhakikisha maeneo yaliyotengwa kwa uwekezaji yanatumika kama ilivyokusudiwa. 

“Hakuna sababu kwa wawekezaji kusumbuliwa kwa sababu serikali inatumia nguvu kubwa kuwavutia kuja nchini kwa maendeleo ya taifa letu,” amesema Rais Samia, huku akilaani tabia ya baadhi ya viongozi wa halmashauri kujihusisha na vitendo vya rushwa kwa wawekezaji wa ndani.

Amezitaka halmashauri kutumia utawala wa sheria katika kushughulikia wawekezaji wanaokiuka makubaliano ya uwekezaji ili kuepusha hasara kwa serikali. Pia alisisitiza umuhimu wa kushirikiana na Mwanasheria Mkuu wa Serikali katika kushughulikia migogoro ya uwekezaji.

Ameagiza halmashauri kuhakikisha kuwa mipango yao inaendana na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050. Pia aliwataka viongozi wenye nia ya kugombea nafasi za kisiasa katika Uchaguzi Mkuu ujao kutoa taarifa mapema ili serikali iweze kupanga mbadala wao.

“Kiongozi yeyote anayepanga kugombea ahakikishe anatoa taarifa mapema. Wale watakaogombea bila taarifa na wasifanikiwe, watajiondoa wenyewe kwenye utumishi,”amesema Rais Samia.

Katika hatua nyingine,amezipongeza halmashauri za Ludewa, Tanganyika, na Kwimba kwa matumizi bora ya mapato na ubunifu wao katika kuboresha huduma kwawananchi. Aliwataka wakurugenzi wa halmashauri kote nchini kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kuhakikisha wananchi wanapata huduma stahiki bila usumbufu.

Matangazo

  • MAPATO YA NDANI YA HALMASHAURI. March 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Rais Samia Aziagiza Halmashauri Kusimamia Mapato na Matumizi Sahihi

    March 13, 2025
  • ALAT yaipongeza Serikali kwa Maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa

    March 11, 2025
  • Waziri Mchengerwa awataka Viongozi wa Mitaa kusukuma maendeleo katika maeneo yao

    March 12, 2025
  • NMB Yadhamini Mkutano Mkuu wa 39 wa ALAT kwa Sh Milioni 170

    March 10, 2025
  • View All

Video

mikumi
More Videos

Quick Links

  • ALAT

Related Links

  • TAMISEMI
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Jengo la Sokoine,Barabara ya CDA Dodoma

    Postal Address: P.O.Box 2049 DODOMA

    Telephone: 0262323407

    Mobile: +255(0)784209840 au

    Email: alat_tz@yahoo.com

Mawasiliano mengine

   

Wanaotembelea

Visitors Counter

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2018 ALAT . All rights reserved.