• complaint |
    • Wasiliana nasi |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
ASSOCIATION OF LOCAL AUTHORITIES OF TANZANIA-ALAT
ASSOCIATION OF LOCAL AUTHORITIES OF TANZANIA-ALAT

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania

  • Home
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Mission and Vision
  • Tunafanya nini?
    • Service one
    • Services two
  • Utawala
    • Organization Structure
  • Machapisho
    • Guidelines
    • Procedures
    • Reports
    • Utawala
    • Application Forms
  • Kituo cha Habari
    • Press Release
    • Videos
    • Speeches
    • Photo Gallery
    • Habari Mpya
    • Matukio
  • Projects
    • lic projects
  • Halmashauri

ALAT yaipongeza Serikali kwa Maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa

Posted on: March 11th, 2025

Na Mwandishi wetu, Dodoma

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), Mhe. Murshid Hashim Ngeze, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa juhudi kubwa inazochukua katika kuboresha huduma za kijamii na kuendeleza miradi mikubwa inayofaidisha wananchi.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa 39 wa ALAT uliofanyika tarehe 11 Machi, 2025 katika Ukumbi wa Jakaya Mrisho Kikwete Convention, Jijini Dodoma, Mhe. Ngeze ametaja mafanikio mengi yaliyopatikana chini ya uongozi wa Rais Samia SuluhuHassan.

 Ameeleza kuwa miradi mikubwa kama reli ya kisasa (SGR), bwawa la Mwl. Julius Kambarage Nyerere, na miundombinu mingine imechangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi na kuboresha maisha ya Watanzania, na kwamba miradi hii inatoa fursa nyingi za ajira namaendeleo kwa jamii.

Aidha, Mhe. Ngeze amesisitiza umuhimu wa miradi hiyo katika kuongeza ufufuaji wa uchumi na ustawi wa wananchi, akisema kuwa hatua hizo zinaonyesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kutatua changamoto za kijamii na kiuchumi. 

Ameongeza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya uongozi thabiti wa Rais Samia na juhudi zake za kuhakikisha kuwa miradi mikubwa inatekelezwa kwa ufanisi, ikilenga kuboresha huduma za kijamii na kuleta maendeleo endelevu katika maeneo yote ya nchi.

Mhe. Ngeze amesema ALAT imeendelea kutekeleza majukumu yake ya msingi, ikiwa ni pamoja na usimamizi wa wanachama wake, uwakilishi wa maslahi ya Serikali za Mitaa kimataifa, na kutoa huduma bora kwa wananchi kupitia mafunzo na usambazaji wa habari muhimu. 

Amepongeza Serikali kwa kutenga fedha nyingi kwa ajili ya miradi ya maendeleo katika sekta za afya, elimu, barabara,na kilimo, na kuongeza kuwa juhudi hizi zimeleta mabadiliko makubwa katika maisha ya Watanzania.

Aidha, amesisitiza umuhimu wa kushirikiana kwaumoja na uadilifu katika mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa 2025, akitoa wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha na kuchagua viongozi bora kwa ajili ya maendeleo endelevu ya nchi. 

Mhe. Ngeze ameishukuru Serikali kwa msaada mkubwa katika maandalizi ya mkutano huo, na kutoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, kwa ushirikiano wake mkubwa.



Matangazo

  • MAPATO YA NDANI YA HALMASHAURI. March 17, 2022
  • View All

Latest News

  • Rais Samia Aziagiza Halmashauri Kusimamia Mapato na Matumizi Sahihi

    March 13, 2025
  • ALAT yaipongeza Serikali kwa Maendeleo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa

    March 11, 2025
  • Waziri Mchengerwa awataka Viongozi wa Mitaa kusukuma maendeleo katika maeneo yao

    March 12, 2025
  • NMB Yadhamini Mkutano Mkuu wa 39 wa ALAT kwa Sh Milioni 170

    March 10, 2025
  • View All

Video

mikumi
More Videos

Quick Links

  • ALAT

Related Links

  • TAMISEMI
  • NECTA

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Jengo la Sokoine,Barabara ya CDA Dodoma

    Postal Address: P.O.Box 2049 DODOMA

    Telephone: 0262323407

    Mobile: +255(0)784209840 au

    Email: alat_tz@yahoo.com

Mawasiliano mengine

   

Wanaotembelea

Visitors Counter

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service

Copyright ©2018 ALAT . All rights reserved.